latest Post

AINA TANO ZA MAZOEZI YA KUJAZA NA KUTANUA KIFUA BILA VIFAA VYA UZITO


Watu wengi wamekua wakiniuliza ni namna gani mtu anaweza kujenga misuli ya kifua bila ya kubeba vitu vizito, basi leo ntagusia swala hilo na natumae litawasaidia. Kifua kimejengwa na misuli iitwayo pectoralis major  ambayo ipo karibu na torso(munganiko wa mabega na mikono). Kikubwa kinachohitajika ni kufanyisha mazoezi yakutanua misuli hyo eidha kwa kutumia vifaa vizito ama mazoezi ya kutumia mwili pekee. Sasa basi leo tutaongelea njia ya kukuza misuli hiyo ya kifua kwa kutumia mwili pekee, na njia hizo ni;



  •  Pushups za kawaida

Push ups za kawaida uhitaji mtu kusukuma mwili kutoka chini na kuiweka nyuzi tisini(90*), ambapo itakuhitaji ufanye marudio kulingana na idadi utakayo pendelea kufanya. Hili zoezi husaidia kukaza misuli ya kifua na pia kutengeneza muonekano mzuri wa kifua.


  •  pushups za inklin 

Hii ni aina ya pushup inayo muhitaji mtu aweke mikono pahali pajuu palipo inuka kidogo kutoka chini(kama mita moja) nakuweka mikono nyuzi tisini(90*) kutoka pahali ulipoweka viganya vya mikono. Zoezi hili lina kulazimisha kujinyanyua juu na chini, kwa mizunguko kadha(set) kwa idadi(count) unazozitaka...Hili zoezi hugusa kwenye wsala kubwa lakukaza misuli ya mikono(bicep na tricep) na pia kutengeneza kifua cha chini.


  • Pushups za muinuko
Hii ni aina ya pushup inayo muhitaji mtu aweke mikono pahali palipo shuka kutoka sehemu ulipo weka miguu. Hapo inampasa mtu aweke mikono chini ikiwa imekaa usawa wamabega na nyuzi tisini(90*) kutoka chini Zoezi hili lina kulazimisha kujinyanyua juu na chini, kwa mizunguko kadha(set) kwa idadi(count) unazozitaka.Hili zoezi hugusa kwenye wsala kubwa lakukaza misuli ya mikono na pia kutengeneza kifua cha juu



  • Zoezi la kujivuta juu
Hili zoezi humuhitaji mtu kujishikilia pahali pa juu palipo inuka ambapo miguu haigusi chini kirahisi, na kujishkiza mikoni kwenye sehemu kama vile(chuma). umuhimu wa zoezi hili ni kwamba husaidia kuvuta kifua cha juu( chini ya kidevu) na hivyo kuweka muonekano mzuri wa kifua.


  • Zoezi la kujididimiza
Zoezi hili lina muhitaji mtu adidimize mwili(katikati) kwanzia kiuno mpaka miguu chini huku akijishkiza mikono yake pande mbili( kulia na kushoto) kwenye vyuma viwili tofauti. Zoezi hili husaidia kukaza misuli chini ya torso itwayo litissimal dorsi ambayo huchangia zaidi kwenye muonekano wa kifua.
Mazoezi hayo yote huwezekana kufanyika sehemu yoyote pale kwa sababu haitaji uzito wowote ule na pia haikulazimu kuingia GYM ili ufanikishe hilo.
Kwa maoni ama ushauri tafadhali tuandikia chini baada ya andiko hili, na kama umeipenda pia weza kutuandikia.

Tafadhali kwa maswali zaidi usisite kutuandikia ama kutupigia kwa number (0653009477) na pia waweza kutufwalia kwenye mitandao ya kijamii kama vile (Twitter, Instagram na Facebook)

About Kuafit

Kuafit
Recommended Posts × +

26 comments:

chandonya alisema ...

kaka ben sasa haya mazoez unafanya kwa mda gani kuanza kuona mabadiliko.🤔🤔

Kuafit alisema ...

Mazoezi haya hutegemea na ufanyaji wako, kwa wale wanaotaka kuanza mazoezi wanaweza kuanza na push-ups za kawaida kwanza kwa siku one mpaka sita, ilikuongeza nguvu kwenye mikono kwa mizunguko miwili kwa hesabu ya tano kila mizunguko. Pili waweza kuanza kufanya mazoezi yote kwa mzunguko mmoja kwa hesabu ya tano kwa kila zoezi moja kwa wiki moja na siku mbili. Tatu waweza kuongeza idadi kwa kufanya mizunguko kuwa miwili kwa kila zoezi kwa hesabu za tano kwa kila mizunguko kwa wiki mbili. Pia waweza kuongeza idadi kulingana na uwezo wako wakufanya mazoezi, yaweza kumchukua mtu siku thelathini mpaka arobaini kuona mabadiliko.....
Natumae maelezo haya yamekusaidia ndugu..Chandonya

Unknown alisema ...

Kaka mm ninataka kuja kifua Na misuli ya mikono je n pushap ngap kwa siku ambazo zina weza kusaidia kuja kifua kwa urahisi Na muda mfup

Unknown alisema ...

Je ukitak kujaz kifua.kwa pusha?

onesmo kaaya alisema ...

nimeipenda hiyo, uko vema sana kaka

Unknown alisema ...

Mm Hupenda Kufanya Mazoez usiku.Je Nisahihi??

Unknown alisema ...

Kaka mm Kira bada yasiku mbili napiga 300 mpaka 500 rakini bado sijalizika namapadiliko ninayo yaona kwani naona Kama bado nimadogo sana nishauli niongezee nanini tena

Unknown alisema ...

GD

Bila jina alisema ...

Je, ukifanya yote hayo misuli ya mikono nayo hupanuka au ni chest pekee?

Unknown alisema ...

kwaiyo inatkiw kufanya mal ngap kwa siku

Unknown alisema ...

Mm nataka kupasua kifua

Unknown alisema ...

Nataka kupasua kifua

Unknown alisema ...

Aanh upo vizr kaka, wacha tufanyie kazi

Unknown alisema ...

Clamency

Unknown alisema ...

nenda muimbili

Unknown alisema ...

Saf sana nimeipenda hiyi

Kuafit alisema ...

Karibu sana

Kuafit alisema ...

Hahahahaha

Unknown alisema ...

Mimi nashauri utoe elimu pia ta kurudisha kifua kilicho jaa kiwe cha kawaida.

Unknown alisema ...

Kaka nakama KIFUA chako kina manyama Sana hasa Kwa MTU mnene kiasi ...pushap xinaweza saidia kuxikaza nyama za kifua

Wihirirya alisema ...

Ahsante vp kuhusu squat

Unknown alisema ...

Kaka je una mshaura nn MTU anayetaka kutengeneza kifua kwa haraka aende gym au afanye workout tu nyumbn na pia VIP kuhusu powder wanayotumia watu wanofanya mazoez

Kuafit alisema ...

Mtu anayetaka kujenga misuli anaweza Jenga mahala popote Ila atabidi apate mwalimu mzuri na pia mazingira na vifaa muhimu kujenga misuli

Kuafit alisema ...

Ukiangalia vizuri kwenye site yetu utaona Kuna chapisho juu ya mazoezi ya miguu ambayo yatakufaa Sana

Kuafit alisema ...

Push-up tu haitoshi Bali pia mazoezi ya kupunguza mwili Kama kukimbia ni muhimu

Kuafit alisema ...

Shukrani kwa mchango wako

KUPUNGUZA UZITO KWA MAJI YA BARIDI

Watu wengi katika jamii hupendelea kuoga na maji ya moto katika majira yote ya hewa lakini kutokana na utafiti uliofanywa na wanasayansi kam...