latest Post

TIBA YA NGUVU ZA KIUME



         Ni kweli kwamba katika jamii yetu kumetokea  malalamiko mengi kuhusiana upungufu wa nguvu za kiume, hii ya weza kusababishwa na mambo kama vyakula vilivyotengenezwa viwanadani vilivyoundwa na sodium kwa kiasi kikubwa ama majera sehemu ya uzazi na hata sababu nyingine za kiafya.
Kutokana na shida hiyo madaktari wamelazimika kutengeneza dawa ambayo inayoweza kuondoa tatizo hilo kwa wanaume wenye shida hiyo ili kuwewezesha kumudu mahusiano yao na wapenzi wao.
Dawa hizo za viagra amabazo hupatikana kwa vidonge  hupatikana lakini kwa gharama , kwa sababu hiyo ililazimika kutafuta njia mbadala na ya urahisi ambayo itakayo mwezesha mtu yeyote kumudu kwa njia asilia kutengeneza viagra.
       Viagra asili hutumia matunda asilia ambayo yakiandaliwa vizuri na kwa kiwango sahihi huweza kuleta mabadiliko muhimu yanayohitajika na mwili ili kukabiliana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.
Matunda yanayotumika kutengeneza viagra hupatikana kiurahisi katika masoko yetu na kwa bei nafuu , matunda hayo ni Tikiti_maji, Limao, Beetroots na Strawberry. Mchanganyiko huo waweza kutengenezwa kwa maelekezo yafwatayo

Kwanza osha na kata tikiti lako robo tatu ama zima kwa kutegemea ukubwa wa tikiti , weka tikiti ulilolikata kwenye mashine yako ya kusaga(blenda) bila kutoa matetere yake,  hakikisha usiongeze kitu cha aina yoyote kama vile sukari na ukishamaliza saga mpaka juisi kutengenezeka.

Baada ya hapo weka juisi hiyo kwenye sufuria na anza kuchemsha juisi hiyo ya tikiti kwa moto wa wastani huku ukisubiria kuweka juisi ya matunda mengine. 
Kamulia limao kwenye juisi ya tikiti bila kusahau kutoa matetere yake wakati ikiwa inachemka, kamulia angalau limao moja ama moja na nusu. Chemsha mchanganyiko huwo kwa dakika kadha hadi bakize nusu ya kiasi cha juisi uliyoweka awali na iache juisi hiyo ipoee kwa dakika thelathini(30).
Ukiwa unasubiria juisi ipoe katakata tunda la beetroot moja katika vipisi vidogodogo na kisha weka kwenye mashine yako ya kusagia matunda.
Baada ya kuweka beetroot kwenye mashine yako kata strawberry nne kwa vipisi vidogovidogo bila kusahau kutoa sehemu iliyokuwa ngumu,

 na kisha tia maji kama glass ya kati moja kwenye mashine na kisha washa mashine ili mchanganyiko usagike pamoja.
Baada ya hapo chuja mchanganyiko wako beetroots na strawberry na chujio safi  na kisha changanya juisi uliyoichuja na juisi ya mchanganyiko wa tikiti na limao angali bado ya vuguvugu kisha koroga kwa mda mrefu ilikuhakikisha mchanganyiko huo umechangamana vizuri na kisha hifadhi sehemu bardi tayari kwa kunywa.
     Juisi ya mchanayanyiko wa matunda hayo manne  ni nzuri hasa kwa watu wenye matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume, kutokana na kuwa na upatikanaji wa citrulline na lycopene kutoka kwenye tikikiti na limao pamoja potassium na nitrate kutoka kwenye strawberry na beetroots. 

  Juisi hii yapaswa kunyweka asubuhi kabla ya kunywa chai ama chakula chochota na pia jioni kabala ya chakula cha jioni ili kufanya kazi kikamilifu.

Kama umeipenda andiko hili basi gonga NZURI  na  kwa maswali na maoni zaidi basi tuandikie baada ya andiko hili, na pia kama ungependa kusoma andiko jengine kama hili basi jisajili kwa kuweka anuani yako  kwenye linki ya SUBSCRIBE.
Pia waweza tuandikia kwa email yetu Kuafit08@gmail.com
Kwa number yetu ya Tigo +255653009477
Instagram account yetu  (KUAFITI), Facebook-(kuafit),

 twitter-(kuafit) 










About Kuafit

Kuafit
Recommended Posts × +

0 comments:

KUPUNGUZA UZITO KWA MAJI YA BARIDI

Watu wengi katika jamii hupendelea kuoga na maji ya moto katika majira yote ya hewa lakini kutokana na utafiti uliofanywa na wanasayansi kam...