latest Post

UFANYWAJI WA MAZOEZI YA KUJENGA MISULI KULINGANA NA AINA YA MWILI



Kwenye ufanyaji wa mazoezi ya kujenga misuli Kuna Mambo kadhaa ya kuzingatia na Mambo haya ni pamoja na kiwango cha chakula kulingana na aina ya chakula( mfano -wanga, vitamini, protini) na hii ni bila kusahau umuhimu wa kuzingatia ukubwa wa mwili.



Watu wengi wakiwa wanafanya mazoezi ya kujenga misuli hupuuza umuhimu wa kuzingatia ukubwa wa mwili na hivyo hupelekea mtu kutopata matokeo mazuri na hata pia kutokuona matokeo kabisa

Inafahamika kwamba Kuna aina 3 ya miili ikiwemo 


  1. Ectomorph - ni aina ya mwili ambapo mtu huwa mwembamba na hujaza misuli lakini kwa shida na kwa kazi kubwa
  2. Mesomorph - ni aina ya mwili wa wastani ambapo mtu huweza kuongeza misuli kirahisi ukilinganisha na makundi mengine
  3. Endomorph - Aina hii ya mwili huwa mkubwa na mwili wa haina hii huwa ni mrahisi kuongezeka kutokana na seli za mafuta hivyo kupelekea mtu kuwa mnene asipokuwa mwangalifu


Nb: mwili wa mtu mmoja unaweza ukawa unatabia zaidi ya moja mfano:- ( mtu mmoja anaweza akawa na 3% mesomorph, 2% ectomorph na 5% endomorph). Kutokana mfano huo mtu huyo atakuwa amesimamia zaidi katika upande wa kuongezeka. Vipimo hivyo vinaweza fanyika mahabara ama mtu anaweza chukua nafasi kuusoma mwili wake kwa kucheza na chakula kwa kula kiasi kidogo na kingi ili kuona mwili unvyopungua na kuongezeka.

Hivyo ufanywaji wa mazoezi wa watu lazima utofautiane hasa kwenye swala la unyanyuaji wa vyuma vizito na mazoezi ya cardio(mazoezi ya kujenga pumzi na kupunguza mwili kama kukimbia nakadhalika)  kamaifwatavyo-





  • Ectomorph - Kwenye ufanyaji wa mazoezi wa mtu wa kundi hili hulazimika kufanya mazoezi ya kunyanyua uzito kwa kiasi kikubwa kuliko mazoezi ya cardio. Endapo mtu wa kundi hili ataongeza mazoezi ya cardio kuliko ya kunyanyua uzito basi mwili wake utapungua Sana. Mtu wa kundi hili hupaswa kufanya mazoezi ya kunyanyua uzito angalau mara tano (5) hadi  sita (6) kwa wiki na mda usiopungua lisaa na robo.


  • Mesomorph - Watu wa kundi hili huwa urahisi mkubwa Sana kwenye kuongezeka misuli kuliko kundi lingine. Hivyo mtu wa kundi hili hushauriwa kufanya mazoezi kulingana na mahitaji yake ikimaanisha Kama anatamani kuwa na mwili mkubwa Sana atalazimika kufanya mazoezi kwa mda wa lisaa na nusu lakini endapo atakuwa na hitaji lakuongezeka kidogo basi atapaswa kutofanya mazoezi kwa mda wa lisaa kwa siku na ni kwa siku nne(4) hadi tano (5) ndani ya wiki. Ufanywaji wa cardio utategemea na kiwango cha mafuta aliyokuwa nacho na kwa maranyigi huwa ni kiwango cha kawaidi hivyo inawezekana ikawa Mara tatu (3) hadi nne (4) wiki.



  • Endomorph - kundi hili la watu hulazimika kufanya mazoezi ya cardio na kunyanyua uzito kwa viwango sawa maana watu Hawa huwa na seli za mafuta nyingi. Ufanyaji wake wa mazoezi hautofautiani na mesomorph kwenye unyajuaji uzito Bali kwenye mazoezi ya cardio ambapo watu wa kundi hili hulazimika kufanya mazoezi ya cardio sio chini mara sita (6) kwa wiki na kwa dakika thelathini (30) kwa siku


Mambo haya ndio yamsingi Sana kuzingatia pamoja na mlo sahihi ili kupata matokeo mzuri.

Kama umeipenda andiko hili basi gonga NZURI  na  kwa maswali au maoni zaidi basi tuandikie baada ya andiko hili, na pia kama ungependa kusoma andiko jengine kama hili basi jisajili kwa kuweka anuani yako  kwenye linki ya SUBSCRIBE. 
Pia waweza tuandikia kwa email yetu Kuafit08@gmail.com 

Kwa number yetu ya Tigo +255 653 009 477  

Instagram account yetu  (KUAFITI), Facebook-(kuafit) na twitter-(kuafit)


About Kuafit

Kuafit
Recommended Posts × +

0 comments:

KUPUNGUZA UZITO KWA MAJI YA BARIDI

Watu wengi katika jamii hupendelea kuoga na maji ya moto katika majira yote ya hewa lakini kutokana na utafiti uliofanywa na wanasayansi kam...