"Furaha ni maana halisi na kusudi la maisha, ni mjumuisho wa kusudi la kuwepo kwa mwanadamu"
mwanafalsafa Aristotle alisema maneno haya zaidi ya miaka 2000 iliyopita and mpaka sasa bado yanaukweli ndani yake.Furaha ni mada pana ambayo inaelezea kuwa na hisia nzuri (positive emotion) kama vile kutosheka na kuridhika.Tafiti nyingi zinaonyesha kuwa mtu mwenye furaha haikufanyi ujisikie vizuri tu bali huleta faida kubwa katika afya yako.
Furaha na Afya njema huwa vinaendana pamoja, tafiti za kisayansi zinaonyesha kuwa na furaha huleta faida katika afya ya moyo na kuboresha mfumo wa kinga mwilini na kuishi maisha marefu.
Pia inaonyesha kuwa na furaha husaidia kupata usingizi mzuri ambao utakuwezesha kuwa na uwezo mzuri wa kufikiri,uzalishaji bora katika kazi zako pamoja na kuwa na uzito wa wastani.
utafiti uliofanyika kwa watu wazima 700 unaonyesha asilimia 47 ya watu wote walikuwa na matatizo ya kupata usingizi na kuwa na usingizi wa kukatika katika mara kwa mara kutoka na kuwa na kukosa hali nzuri ya kuwa na furaha.
SABABU ZA KUWA NA FURAHA ILI kUBORESHE AFYA YAKO
1.Kuboresha mfumo wa kinga mwilini
Kuwa na mfumo mzuri wa kinga mwilini ni jambo la muhimu sana kwa sababu hutusaidia kutukinga na magonjwa mbalimbali.Tafiti zinaonyesha kuwa na furaha mara kwa mara husaidia kuboresha nguvu ya kinga mwilini na kupunguza kupata magonjwa ya mafua pamoja maambukizi ya kifua.
2. Husaidia kulinda Moyo wako
Furaha huchangia pia katika kuboresha afya ya moyo wako wa kupunguza presha ya damu ambayo huchangia mtu kupata magonjwa ya moyo.Utafiti uliofanyika kwa watu 6500 wenye zaidi ya miaka 65 ulionyesha watu wenye hali nzuri na furaha walikuwa na asilimia 9 ya kuwa na presha ya damu ya kiwango cha juu (high blood pressure)
Pia kuwa na furaha uchangia kupunguza kupata magonjwa mbalimbali ya moyo ambayo husababisha vifo vingi duniani.3.Kurefusha maisha.
Mara nyingi watu ambao huwa na furaha huishi kwa muda mrefu hapa duniani.Hi uchangiwa na hali kujihusisha katika shughuli mbalimbali ambazo huboresha afya zao.Mfano kupenda kufanya mazoezi.
4.Kupunguza msongo wa mawazo
Kuwa mtu wa furaha pia husaidia kupunguza kuwa na msongo wa mawazo. Kikawaida mtu mwenye msongo wa mawazo huchangia kudhoofisha afya ya mwili na kupata magonjwa mbalimbali kama vile type 2 diabetes na kuwa na presha ya damu ya kiwango cha juu (high blood pressure).5.Kupunguza maumivu
Kuwa na furaha katika nyakati tofauti pia husaidia kupunguza hali ya kujisikia maumivu mwilini. furaha husaidia kupunguza hali ya kuwa na maumivu sugu (chronic pain) ambayo hushambulia sehemu za muunganiko(joint) kitaalamu inaitwa arthritis.
Baada ya kujua faida za kuwa na furaha ni vyema ukajua na namna gani ukaanza kuongeza hali ya kuwa na furaha katika maisha yako ambayo itaboresha afya yako.
1.Fanya mazoezi
Mazoezi aina ya Aerobic au Cardio huchangia sana mtu kuwa na furaha.Kupenda kutembea (dakika 30) au kucheza mchezo unaopenda haitachangia kuboresha afya yako ya mwili pia itaboresha kuwa na hali nzuri na furaha zaidi2.Pumzika vya kutosha
kukosa usingizi wa kutosha uchangia mtu kukosa furaha .Unashauriwa kupata muda mzuri wa kupumshiza mwili na akili yako, hii husaidia mwili na akili yako kufanya kazi vizuri pale unapoamka asubuhi.
3.Fanya Tahajudi(meditation)
kufanya tahajudi mara kwa mara huchangia kuongeza hali ya kuwa na furaha katika maisha yako,pia huchangia kupunguza hali ya kuwa na msongo wa mawazo.Kama hujuia namna ya kufanya tahajudi soma makala hii aina za tahajudi4.Kula chakula bora
Unashauriwa kutokula chakula bila mpangilio maalumu kwani husababisha afya yako kuzorota.Tafiti zinaonyesha ulaji wa matunda na mboga za majani mara kwa mara uchangia mtu kuwa na hali ya furaha5.kuwa mtu wa shukrani
Hali ya kushukuru kwa yale mema yalitokea katika maisha yako uchangia kiasi kikubwa kuwa na furaha.Njia mojawapo ya kukuwezesha kuonyesha hali ya shukrani ni kuandika mambo matatu yaliyochangia kuwa na hali nzuri katika siku hiyo.
Kama umeipenda chapisho hili basi gonga NZURI na kwa maswali au maoni zaidi basi tuandikie baada ya andiko hili, na pia kama ungependa kusoma andiko jengine kama hili basi jisajili kwa kuweka anuani yako kwenye linki ya SUBSCRIBE.
Pia waweza tuandikia kwa email yetu Kuafit08@gmail.com
Kwa number yetu ya Tigo +255 653 009 477
Instagram account yetu (KUAFITI), Facebook-(kuafit)
0 comments:
Chapisha Maoni