latest Post

MAZOEZI ANAYOWEZA KUFANYA MWANAMKE MJAMZITO KULINGANA NA WIKI ALIZOFIKIA


 Kikawaida ujauzito kwa mwanamke hudumu ndani ya wiki 40 ambapo kwa jumla ni sawa na miezi tisa. Ndani ya kipindi hicho mwilii wa mwanamke hupata mabadiliko mengi ambapo hutokana na ukuaji wa mtoto ndani ya tumbo la uzazi. Mabadiliko hayo ndani ya mwanamke mjamzito kwa kitaalamu hutokea kwa vipindi vitatu ambavyo ni kipindi cha kwanza (first trimester), kipindi cha pili( second trimester), kipindi cha tatu( third trimester). Ni ndani ya vipindi hivi ambapo mtoto huchukua hatua ndogo ngogo za ukuaji na vipindi hivi hufahamika kulingana na wiki ambazo mwanamke mja mzito amezifikisha.
Ni kweli kwamba kuna haja kubwa ya wanawake wajawazito kufanya mazoezi kutokana na kwamba miili yao huitaji kuwa na nguvu na imara ili afaya ya mtoto iweze kuhimarika pia.
Tazama faida ya wanawake wajawazito kufanya mazoezi

Ukuaji wa mtoto ndani ya mwanamke mjamzito huathiri mwili wa mwanamke kwa namana nyingi kama vile uvutaji pumzi, mzunguko wa damu, mapigo ya moyo na pia bila kusahau upanganyikaji wa misuli ndani ya mwili wake.
Mazoezi kwa wanawake wajawazito hupaswa kufanywa kwa kuzingatia vipindi vitatu vya ujauzito kama nilivyo elezea awali. Ndani ya vipi hivyo vitatu mwanamke mjamzito anapaswa kufanya mazoezi kulingana na kipindi alichopo ili aweze kupunguza uwezekano wa majeraa kutokana na mabadiliko yaliyoletwa na ujauzito pia kuepusha kuhatarisha maisha ya mtoto.


  • Kipindi cha kwanza(first trimester)
   Hutokea kwanzia pale mtoto anapotungwa tumboni mwa mama yake mpaka wiki ya 12. Ndani ya wiki hizo kumi na mbili ndipo mgongo na ubongo huanza kujitengeneza kwa mtoto tumboni na pia misuli inayotengeza umbo lake huanza kuonekana. Mwanamke mjamzito ndani ya wiki hizi kumi na mbili asiye na historia ya kufanya mazoezi  anashahuriwa kufanya mazoezi ya kawaida  kama vile;-

-Yoga

ambapo atanyoosha misuli ya mwili na kumfanya ajisikie vizuri na mwenye afya

-Kutembea

ambapo kwa kutembea kutamfanya aweze kupunguza uwezekano wa mwili wake  kuvimba kwa kukaa sehemu moja na pia kujenga pumzi.

-Kucheza aerobics

kwa kufanya mazoezi ya aerobics kutamwezesha kufanyisha moyo mazoezi kwa  kusukuma damu kwa wingi na pia  kutamsaidi  kutokuvimba kwa mwili

  Kwa mwanamke mwenye uzoefu katika ulimwengu wa mazoezi anaweza akafanya mazoezi zaidi kuliko mwanamke ambaye hana historia ya kufanya mazoezi. Mazeozi ya nyongeza ukitoa yale ambayo mwanamke asiye nahistoria ya mazoezi anayoweza kufanya ni kama vile;-

-Squat

ambapo kwa kufanya hili mwanamke mja mzito mwenye uzoezi wa mazoezi anaweza   akajenga nguvu zaidi ya miguu.

- Kunyanyua vyuma 

 ndio! kwa mwanamke mwenye ujuzi wa mazoezi aliyekuwa mjamzito  anaweza kunyanyua vyuma vyenye uzito mdogo ili kuongeza nguzu na kukaza misuli(toning) na pia viungo vya mwili.

-Kuogelea

kwa kufanya mazoezi ya kuogelea mwanamke mjamzito anweza kuongeza nguvu ya viungo vyake vya mwili na pia kujenga pumzi.


  • Kipindi cha pili(second trimester) 
Kipindi hiki hutokea kwanzaia wiki ya 13 na humalizika hadi wiki ya 27. Ndani ya kipindi hiki ndipo mtoto anpoanza kuongezeka misuli ya mwili wake, ngozi yake huanza kuonekana na pia mwili wa mtoto hukua ahadi inch 4 mpaka 5. Mwanamke mja mzito ndani ya kipindi hiki huonekana kuwa na tumbo kubwa kidogo ukilinganisha na kipi cha kwanza, na pia mazoezi anyopaswa kufanya ni machache ukilinganisha na mazoezi ya kipindi cha kwanza. Mazoezi anayoweza kuafanya mwanamke mjamzito ndani ya kipi hiki ni;-

-Mazoezi ya kujinyoosha

kwa kuanfya mazoezi ya kujinyoosha(stretching) kunaweza kuweka mwili  wake katika hali nzuri ambapo hatopata maumivu ya viungo kama vile mgongo na mengineyo.

-Kutembea

kwa kufanya mazoezi haya ya kutembea kunaweza kumsaidia mjamzito kutokuvimba kwa miguu yake na pia kusaidia kwenye swala la pumzi.

-Yoga 

kutokana na ukubwa wa tumbo kwa kipindi hiki na kushindwa kufanya mazoezi mengi kwa mama mjamzito basi ni vyema kufanya zoezi hilli ili aweze kujinyoosha na kutengeneza afya nzuri ya akili yake mbali na msongo wa mawazo.

-Mazoezi ya kucheza muziki

mwanamke mjamzito anaweza akafanya mazoezi ya kucheza muziki kama vile salsa ambapo hatotumia nguvu nyingi ya mwili wake.
  • Kipindi cha tatu(third trimester) 
kindi hiki huanzia kutoka wiki ya 28 na humalizikia wiki ya kujifungua. Ndani ya kipindi hiki ndipo mwanamke mjamzito hula sana kutokana na kwamba umalizikiaji wa ukuaji wa mtoto tumbono hutokea. Kipindi hiki ndipo mwanamke mjamzito anapaswa kuwa mwangalifu ambapo atapswa kupunguza kazi nyingi na mazoezi mazito, na hivyo anapswa kufanya mazoezi marahisi. Mazoezi ambayo anayoweza kufanya mwanamke mjamzito kwa kipindi hiki ni;-

-Kutembea

mwanamke mjamzito ndani ya kipindi hiki hushauriwa sana kufanya mazoezi ya kutembea kwa umbali mdogo ili aweze kupunguza uwezekana wa kuvimba miguu yake, na pia humsaidia kwenye swala la pumzi.

-Mazoezi ya kujinyoosha

 kwa kufanya mazoezi ya kujinyoosha(stretching) kwa mwanamke mjamzito wa kipindi hiki cha mwisho kunaweza kumsaidia mwili wake kwa kuuweka katika hali nzuri ambapo hatopata maumivu ya viungo kama vile mgongo na mengineyo.

ANGALIZO!! Katika kipindi hiki cha ujauzito inashahuriwa yakwamba mwanamke mjamzito asifanye mazoezi ya tumbo hasa zoezi la crunches ili asijeakatengeneza madhara kwa mtoto aliyopo tumboni

Kama umeipenda andiko hili basi gonga NZURI  na  kwa maswali au maoni zaidi basi tuandikie baada ya andiko hili, na pia kama ungependa kusoma andiko jengine kama hili basi jisajili kwa kuweka anuani yako  kwenye linki ya SUBSCRIBE.

Pia waweza tuandikia kwa email yetu Kuafit08@gmail.com 
Kwa number yetu ya Tigo +255 653 009 477  
Instagram account yetu  (KUAFITI), Facebook-(kuafit) na twitter-(kuafit

About Kuafit

Kuafit
Recommended Posts × +

0 comments:

KUPUNGUZA UZITO KWA MAJI YA BARIDI

Watu wengi katika jamii hupendelea kuoga na maji ya moto katika majira yote ya hewa lakini kutokana na utafiti uliofanywa na wanasayansi kam...