Ni kweli kabisa kuwa wanaume wengi hua wanapenda kujenga heshima na kuonekana bora kuliko mwanaume yeyote kwenye maswala ya chumbani. Lakini tatizo la upungufu wa nguvu za kiume ni janga ambalo hukumba asilimia kubwa ya wanaume duniani, na madhara yake hupelekea hadi kuvunja mahusiano baina yao na wapenzi wao.
Basi leo nitaongelea tunda la BEET na juice yake, pia ntagusia umuhimu wa tunda hilo kwa mwili wa mwanaume. Tunda la beet ni tunda ambalo lina patikana sana katika jamii mbalimbali duniani, na pia watu hutumia tunda hilo kwenye kupika vyakula. Ingawa wengi hutumia kwa matumizi mengine lakini kwa utafiti usio rasmi pia tunda hili lina mchango mkubwa kwenye kuongeza nguvu za kiume. Na inashahuriwa kwa watu wote kutumia ikiwezekana angalau mara tatu kwa wiki juisi ya tunda hili hasa kwa wenye matatizo ya nguvu za kiume .
Faida ya tunda hili la beet ni kama ifwatavyo..
- Hongeza mzunguko wa damu
- Huongeza fiber mwilini
Fiber ni aina ya virutubisho mwilini , virutubisho hivyo ni muhimu sana katika mwili wa mwanadamu ambavyo husaidia katika kupunguza mafuta ya mwili yasio hitajika. Hivyo kwa glasi ya juisi ya tunda la beet basi unauwezekano mkubwa wa kupunguza mafuta ya mwili(choletrol)
- Hutokomeza seli za kansa ya kizazi
- Huongeza virutubisho na madini mbalimbali muhimu
- Huchangia kuwa na ngozi yenye afya
Basi ni wazi kuwa tunda hili la beet lina faidi nyingi sana kwenye kuongeza nguvu za kiume na pia kujenga afya ya mwili. Na kutokana na idadi ya wengi waliotumia utafiti unaonesha asilimia 68% wameona mabadiliko na wanafurahia mahusiano yao kwa sasa.
Kama umelipenda andiko hili basi gonga NZURI na kwa maswali na maoni basi tuandikie baada ya andiko hili, na pia kama ungependa maandiko mengine kama haya basi jisajili kwa kuweka anuani yako juu kwenye linki ya KUJISAJILI
0 comments:
Chapisha Maoni